Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 21, 2013

Boko Haram yaua 19 kaskazini mashariki mwa Nigeria


Boko Haram yaua 19 kaskazini mashariki mwa Nigeria
Watu wasiopungua 19 wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na wanamgambo wa kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa Nigeria. Hayo yameelezwa na wenyeji na watu walionusurika na nmashambulizi hayo. Hadi sasa miili 19 imegunduliwa katika eneo palipojiri mashambulizi hayo ya Boko Haram. Habari zinasema kuwa wanamgambo wa kundi la Boko Haram walifunga barabara kuu karibu na mji wa Logumani umbali wa kilomita 30 kutoka katika mpaka wa Nigeria na Cameroon na kuanza kuua raia na kuchoma moto malori matatu. Wahanga watano ambao miongoni mwao walikuwa ni madereva wawili wa malori na wasaidizi wao waliuliwa kwa kupigwa risasi na waliosalia walichinjwa. Boko Haram imetekeleza mashambulizi hayo jana katika hali ambayo tarehe sita mwezi huu pia kundi hilo liliushambulia msikiti mmoja huko Damboa katika jimbo la Borno na kuwauwa waumini watano waliokuwa katika sala ya asubuhi.