Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 7, 2013

LADY MADONNA AANZA KUJIFUNZA QURANI, NI BAADA YA KUWA NA MAHUSIANO NA KIJANA WA KIISLAMU

Mwanamuziki nyota muziki wa POP duniani Lady madonna
anasema kwa sasa anajifunza kitabu kitukufu cha Qurani na Uislamu.

Madonna ambaye ni mfuasi wa dini ya kiyahudi ya dhehebu la Kabbalah kwa sasa ana mahusiano na mwanaume wa kiislamu Brahim Zaibat ambaye amekuwa chachu ya kuanza kujifunza uislamu.
 

Akizungumza na gazeti la Bazaar Harper alisema Madonna
"Najenga shule kwa ajili ya wasichana katika nchi za kiislamu na nasoma Qurani. Nadhani ni muhimu kusoma vitabu vitakatifu". Madonna amekuwa mfuasi wa dhehebu la Kabbalah tangu mwaka 1996 wakati alipoolewa na mwingereza Guy Ritchie. 


Imeripotiwa kwamba Madonna mwenye umri wa miaka 55, ameanza kujifunza kuhusu uislamu kwa sababu ya mahusiano yake na Brahim Zaibat mwenye umri wa miaka 25. Madonna ambaye amebadilika mno kitabia wengi wanaamini huenda baadae akasilimu.