Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, February 27, 2014

UAMSHO WAACHIWA KWA DHAMANA



MAHKAMA KUU VUGA MJINI ZANZIBAR IMEPUNGUZA MASHARTI MAGUMU YA DHAMANA YALIYOKUWA YAKIWAKABILI VIONGOZI JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU ZANZIBAR YA KULIPA SHILINGI MILIONI 25 NA BADALA YAKE SASA ZIMEKUWA ZA MAANDISHI.

JAJI WA MAHKAMA HIYO FATMA HAMID MAHMOUD AMETOA UAMUZI HUO NA KUSEMA KUWA KUTOKANA NA WATUHUMIWA HAO KUKAA NDANI KWA MUDA MREFU MAHAKAMA IMEONA WANA HAKI YA KUPATIWA DHAMANA.

MASHARTI YENYEWE YALIKUWA NI KUTOA FEDHA TASLIM SHILINGI MILIONI 25, KUWA NA WADHAMINI WATATU WAKIWA NI WATUMISHI WA SERIKALI MMOJA WAO AWASILISHE MALI ISIYOHAMISHIKA PAMOJA NA KUTOSAFIRI NJE YA ZANZIBAR.

HATA HIVYO BAADA YA MAOMBI YA WATUHUMIWA WAKIONGOZWA NA MAWAKILI WAO SALUM TOUFIQ JAJI FATMA ALIKUBALI KILA MSHITAKIWA KUJIDHAMINI KWA SHILINGI MILIONI 25 ZA MAANDISHI PAMOJA NA KUWA NA WADHAMINI WAWILI MOJA AKIWA MFANYIKAZI WA SERIKALI NA WA PILI AWASILISHE MALI ISYOHAMISHIKA BADALA YA WADHAMINI WATATU WAFANYAKAZI WA SERIKALI.

WATUHUMIWA HAO NI AMIRI MKUU WA JUMUIYA YA MAIMAMU ZANZIBAR SAMAHATU SHEIKH FARIDI HADI AHMED,AMIRI MKUU WA JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YAKIISLAM ZANZIBAR FADHILATU SHEIKH MSELEM ALI MSELEM, USTADH MUSA JUMA MUSSA,NAIBU AMIRI WA JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YAKIISLAM ZANZIBAR AL-USTADH AZAN KHALID HAMDAN,KATIBU WA JUMUIYA YA UAMSHO USTADH ABDALLA SAIDI NA MAUSTADHI SLEIMAN JUMA SLEIMAN, KHAMIS ALI SLEIMAN, HASAN BAKARI SLEIMAN, GHARIBU AHMADA JUMA, NA FIKIRINI MAJALIWA .

MASHTAKA WALIOSOMEWA WASHITAKIWA HAO NI KUHARIBU MALI, UCHOCHEZI,USHAWISHI NA KUHAMASISHA FUJO NA KOSA LA TATU NI KULA NJAMA YA KUFANYA KOSA

KOSA LA NNE LIKIMKABILI MSHITAKIWA NAMBA NNE AZAN KHALID AMBAE ANADAIWA KUTOA MANENO YA MATUSI KWA KAMISHNA WA POLISI VITENDO VINAVYOWEZA KUSABABISHA UVUNJIFU WA AMANI.

VITENDO HIVYO VINADAIWA KUFANYIKA KATI YA OKTOBA 17,18 NA 19 MWAKA ,2012 KATIKA MAENEO TOFAUTI KATIKA MANISPAA YAA MJI WA ZANZIBA AMBAPO WASHITAKIWA HAO WOTE WALIKANA MAKOSA YOTE HAYO .

KESI HIYO ILIAKHIRISHWA HADI MACH 27 MWAKA HUU KESI HIYO ITAKAPOSIKILIZWA TENA.

Tuesday, February 25, 2014

TIZAMA PICHA:Maelfu ya wananchi wa mkoa wa Hiraan wajitokeza na kupinga Wanajeshi wa Ehiopia.

Maelfu ya wananchi wa Kislaam wa Somalia wamejitokeza barabarani katika maeneo mbalimbali ya Miji ya Hiraan iliyoko katikati mwa Ardhi ya Somalia.
Maandamano hayo yalikuwa ya kupinga uingiliaji kati na uchokozi ulio wa wazi wa Serikali ya Ethiopia dhidi ya Ardhi ya Kislaam ya Somalia.
Kwenye Barabara ya mji wa Buula Barde walionekana mamia ya Wananchi waliokuwa wakipita kweye Barabara hizo huko wakitamka maneno dhidi ya Adui asilia ya Uvamizi wa Ethiopia aliyovishwa vazi la AMISOM.
Wazee wa koo wa Mkoa wa Hiraan,wanataaluma,walizungumza kwenye Maandamano hayo na kusema kuwa watakuwa tayari kuingia vita itakayochukua muda mrefu dhidi ya wanajeshi wa Ethiopia ili kuilinda Dini na Ardhi yao,waandamanaji wote hao waliokuwa wakipinga Wanajeshi wa Ethiopia kwa ujumla wamekubaliana kuwa Uingiliaji wa Ethiopia uliokuja na sura mpya hautoweza kuathiri chochote harakati iliyokuwa ikiendelea dhidi ya Maadui wa Kigeni walioivamia Rdhi ya Kislaam ya Somalia.

Tuesday, February 11, 2014

Morocco inaamiliana vibaya na wahajiri wa Kiafrika


Morocco inaamiliana vibaya na wahajiri wa KiafrikaShirika la Kutetea Haki za Binadmu la Human Rights Watch limeitaka serikali ya Morocco kuamiliana  kiubinadamu na wahajiri wa Kiafrika wanaopita nchini humo. Taarifa iliyotolewa na shirika hilo imeeleza kuwa, wahajiri wanaopita nchini Morocco wakitokea maeneo ya kusini mwa jangwa la Sahara na kuelekea barani Ulaya, wanakabiliwa na vitendo vya kikatili vinavyofanywa na vikosi vya usalama vya nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kupigwa na kuwekwa rumande bila ya kufunguliwa mashtaka. Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la HRW limeeleza kuwa, licha ya kufanyiwa marekebisho sheria za wahajiri na wakimbizi nchini humo, lakini bado vinaendelea kushuhudiwa vitendo visivyo vya kibinadamu vinavyofanywa na askari usalama  dhidi ya wahajiri.
Wimbi kubwa la wahajiri kutoka kusini mwa jangwa la Sahara limekuwa likipita nchini Morocco na kuelekea Uhispania, lakini limekuwa likikumbana na mateso wakati wa kuondoka nchini humo. Morocco inahesabiwa kuwa kivuko muhimu cha wafanya magendo ya dawa za kulevya na wahajiri haramu ambao hujaribu kuingia Ulaya kinyume cha sheria.

Jeshi la Syria lasisitiza kupambana na magaidi


Jeshi la Syria lasisitiza kupambana na magaidi
Mkuu wa vikosi vya  ulinzi na usalama nchini Syria amesisitiza juu ya kutiwa mbaroni wale wote waliohusika na mauaji ya halaiki ya wananchi wasiopungua 71 wa Syria hapo jana. Mkuu wa majeshi ya Syria ameongeza kuwa, serikali ya Damascus inafanya juhudi za kutatua mateso yanayowakabili  wananchi zinazosababishwa na  njama za baadhi ya mataifa ya nchi za Magharibi na vibaraka wao walioko katika eneo la Mashariki ya Kati. Mkuu wa Majeshi ya Syria amesisitiza kuwa, jeshi la nchi hiyo litaendelea kupambana kikamilifu na kuhakikisha kwamba watenda jinai wa kundi la al Nusra wanahilikishwa kikamilifu.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, magaidi walioko nchini Syria, baada ya kukiteka kijiji cha Maan kilichoko Hamah magharibi mwa Syria waliwauwa kwa halaiki watu 71 wakiwemo wanajeshi 50 wa serikali ya Syria. Mauaji hayo yanatokea katika hail ambayo, leo hii inaanza duru ya pili ya mazungumzo kati ya ujumbe wa serikali ya Syria na wapinzani huko Uswisi.

Ulaya kutuma wanajeshi 500 Jamhuri ya Afrika ya Kati

    Ulaya kutuma wanajeshi 500 Jamhuri ya Afrika ya Kati
Mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje  wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya wamepitisha mpango wa kupelekwa wanajeshi 500 wa umoja huo huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, kwa lengo la kusaidiana na vikosi vya nchi za Kiafrika na vile vya Ufaransa katika kuleta amani nchini humo. Catherine Ashton Mkuu wa Siasa za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, lengo la kutumwa wanajeshi hao ni kutekelekeleza operesheni za kukomesha machafuko na mauaji dhidi ya wananchi wa nchi hiyo na hasa Waislamu ambao wamekuwa wakilengwa na mashambulio ya wanamgambo wa Kikristo wa Anti Balaka. Siku ya Jumapili iliyopita, Shirika la
Kutetea Haki za Bindamu la Human Rights Watch HRW lilitahadharisha kuwa, machafuko yanaondelea kushuhudiwa nchini humo yatasababisha Waislamu wote kuwa wakimbizi.  Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, karibu watu milioni mbili wanahitaji misaada ya kibinadamu nchini humo.

Ikhwanul Muslimin ya Misri yakadhibisha kuunda jeshi

Ikhwanul Muslimin ya Misri yakadhibisha kuunda jeshi
Kiongozi mmoja mwandamizi wa harakati ya Ikhwanul Muslimiin ya Misri amesema kuwa, harakati za kundi hilo zitaendelea kuendeshwa kwa njia za amani na kusisitiza kwamba kundi hilo halina mpango kabisa wa kuanzisha tawi la kijeshi.
Muhammad Ali Beshr amekadhibisha vikali taarifa zilizotolewa na serikali ya Misri kwa vyombo vya habari kwamba, harakati ya Ikhwanul Muslimin imeanzisha tawi la kijeshi kwa lengo la kupambana na polisi na jeshi la nchi  hiyo. Kiongozi huyo mwandamizi wa Ikhwanul Muslimiin amesisitiza kuwa, harakati hiyo itaendelea kupigania haki zake zote kwa njia za amani. Inafaa kuashiria hapa kuwa, hivi karibuni kundi la watu waliobeba silaha lilishambulia kituo cha polisi  na kuwauwa  askari watano na wengine wawili kujeruhiwa. Serikali ya Misri ililifungamanisha shambulio hilo na kundi la Ikhwanul Muslimiin. Wakati huohuo, Mahakama moja nchini  Misri imetoa hukumu ya adhabu ya kifo kwa watu 14 na wengine wanne kifungo cha maisha jela, kwa tuhuma eti walishiriki katika shambulio dhidi ya kituo cha polisi nchini humo.