skip to main |
skip to sidebar
Morocco inaamiliana vibaya na wahajiri wa Kiafrika
Shirika la Kutetea Haki za Binadmu la Human Rights Watch
limeitaka serikali ya Morocco kuamiliana kiubinadamu na wahajiri wa
Kiafrika wanaopita nchini humo. Taarifa iliyotolewa na shirika hilo
imeeleza kuwa, wahajiri wanaopita nchini Morocco wakitokea maeneo ya
kusini mwa jangwa la Sahara na kuelekea barani Ulaya, wanakabiliwa na
vitendo vya kikatili vinavyofanywa na vikosi vya usalama vya nchi hiyo
ikiwa ni pamoja na kupigwa na kuwekwa rumande bila ya kufunguliwa
mashtaka. Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la HRW limeeleza kuwa,
licha ya kufanyiwa marekebisho sheria za wahajiri na wakimbizi nchini
humo, lakini bado vinaendelea kushuhudiwa vitendo visivyo vya kibinadamu
vinavyofanywa na askari usalama dhidi ya wahajiri.
Wimbi kubwa la wahajiri kutoka kusini mwa jangwa la Sahara limekuwa
likipita nchini Morocco na kuelekea Uhispania, lakini limekuwa
likikumbana na mateso wakati wa kuondoka nchini humo. Morocco
inahesabiwa kuwa kivuko muhimu cha wafanya magendo ya dawa za kulevya na
wahajiri haramu ambao hujaribu kuingia Ulaya kinyume cha sheria.
No comments:
Post a Comment