Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 14, 2013

Wawili wauawa kwenye mlipuko Addis Ababa


Wawili wauawa kwenye mlipuko Addis AbabaWatu wawili wameuawa katika mlipuko wa bomu uliotokea mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Jeshi la polisi la Ethiopia limetangaza kuwa, uchunguzi umeshaanza ili kubaini sababu za kutegwa bomu hilo ambalo limelipuka katika eneo la Bole. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na mlipuko huo. Hata hivyo, viongozi wa serikali wanalituhumu kundi la waasi lililoko kusini na kusini mashariki mwa nchi hiyo kwa kuhusika na ulipuaji mabomu nchini Ethiopia.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, mwezi Novemba 2011 Ethiopia ilipeleka vikosi vya dhiba nchini Somalia kwa shabaha ya kulisaidia jeshi la nchi hiyo, kwenye mapambano dhidi ya kundi la al Shabab. Hivi karibuni Hailemariam Deslaegn,Waziri Mkuu wa Ethiopia amesikika akisema kuwa, Addis Ababa haitayaondoa majeshi yake nchini Somalia, hadi pale amani itakaporejea nchini humo.