Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, March 7, 2013

'US, Israel zapanga kuteka maeneo ya mafuta Sudan'


'US, Israel zapanga kuteka maeneo ya mafuta Sudan'Chama tawala cha Kongresi ya Taifa Sudan kimefichua kuwepo njama za mashirika ya kijasusi ya Marekani na Utawala wa Kizayuni ya Israel za kuwaunga mkono waasi nchini Sudan lengo likiwa ni kuyakalia kwa mabavu maeneo yenye utajiri wa mafuta nchini humo.
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, chama hicho tawala nchini Sudan kimesema majasusi wa Israel na Marekani wanaunga mkono makundi ya waasi hasa kundi la JEM la Darfur. Chama cha Kongresi ya Taifa kimesema pamoja na kuwepo oparesheni hizo za majasusi wa Kizayuni na Marekani,
jeshi la Sudan liko macho na litaangamiza njama hizo kikamilifu. Aidha chama hicho kimesema Umoja wa Mataifa umeshatoa ripoti inayoonyesha kuwa serikali ya Sudan Kusini inawaunga mkono waasi wanaoipinga serikali ya Sudan. Hamid Sadiq wa Kongresi ya Taifa amesema ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa imethibitisha ukweli ambao Sudan imekuwa ikiusema mara kwa mara. Wiki iliyopita pia Qutbi al Mahdi mmoja wa viongozi wa chama tawala cha Kongresi ya Taifa ya Sudan alifichua njama za nchi za Magharibi za kutaka kuwalazimisha watu wa Sudan wawe Wakristo sambamba na kuibua hitilafu za kikabila nchini humo lengo likuwa ni kuipokonya nchi hiyo utambulisho wake asili.

No comments:

Post a Comment