Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, March 20, 2013

Polisi ya Misri yamtia mbaroni binamu wa Gaddafi


Polisi ya Misri yamtia mbaroni binamu wa Gaddafi
Polisi ya Misri imesema kuwa imemtia mbaroni binamu na aliyekuwa mpambe wa karibu wa Muammar Gaddafi kiongozi wa zamani wa Libya. Hapo jana maafisa wa Misri walisema kuwa Ahmed Gaddaf al Dam alitiwa nguvuni baada ya vikosi vya usalama kuizingira nyumba yake katika kitongoji cha Zamalek huko Cairo. Afisa mmoja wa Misri amesema kuwa afisa huyo wa zamani wa intelijinsia wa utawala wa Gaddafi atakabidhiwa kwa maafisa wa Libya hivi karibuni. Baada ya kuzingirwa nyumba yake kwa masaa kadhaa huko katikati mwa Cairo, binamu huyo wa Muammar Gaddafi alisikika akizungumza na kanali moja ya televisheni kwa njia ya simu na hapa ninamnukuu" tulifika hapa kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri na baraza la kijeshi, sisi si magaidi wa kuweza kushambuliwa namna hii," mwisho wa kumnukuu.  

No comments:

Post a Comment