Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, March 7, 2013

Berlusconi asukumwa jela mwaka 1 nchini Italia


Berlusconi asukumwa jela mwaka 1 nchini ItaliaMahakama moja nchini Italia imemhukumu Waziri Mkuu wa zamani wa Italia, Silvio Berlusconi kifungo cha mwaka mmoja jela baada ya gazeti lake kupatikana na hatia ya kuchapisha habari ya siri kuhusu shughuli za benki. Hata hivyo, mawakili wa Berlusconi wamesema kiongozi huyo wa zamani hatosukumwa jela hadi rufaa aliyokata itakaposikizwa na kuamuliwa. Iwapo atashindwa kujinasua kutoka kwenye mtego huo, hali ya kisiasa nchini Italia itakuwa chachu kutokana na ukweli kwamba, chama cha Berlusconi ni miongoni mwa vyama vinavyotarajiwa kushirikishwa kwenye serikali ya muungano baada ya wagombea wa wadhifa wa Waziri Mkuu kushindwa kupata ushindi mutlaki kwenye uchaguzi mkuu uliopita.

No comments:

Post a Comment