
Mazungumzo hayo yamefunguliwa na Rais Abdrabuh Mansur Hadi wa nchi hiyo na yanahudhuriwa na zaidi ya wawakilishi 500 kutoka vyama vya kisiasa vya Yemen. Hata hivyo mrengo wa kisiasa wa kusini umesusia mazungumzo hayo na uliitisha maandamano na mgomo katika mji wa Aden hapo jana kupinga suala hilo.
Mazungumzo hayo ni sehemu ya makubaliano yaliyohitimisha utawala wa dikteta Ali Abdullah Saleh ambapo kiongozi huyo aliondoka madarakani na kukabidhi madaraka kwa Abdrabuh Mansur Hadi tarehe 27 Februari 2012.
No comments:
Post a Comment