Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, March 18, 2013

Benki ya Dunia yazisaidia Msumbiji, Malawi na Zambia


Benki ya Dunia yazisaidia Msumbiji, Malawi na ZambiaBenki ya Dunia  kupitia Taasisi ya Maendeleo wa Kimataifa imetoa msaada wa dola milioni 89 kwa serikali za  Msumbiji, Malawi na Zambia kwa lengo la kusaidia  mpango wa chakula salama  na uzalishaji wa kilimo kwenye nchi hizo zilizoko eneo la kusini mwa Afrika.
Hayo yameelezwa na Tijan Sallah Meneja wa Sekta ya Kilimo na Umwagiliaji katika ukanda huo. Sallah ameongeza kuwa lengo la kutekelezwa mpango huo ni kuboresha sekta ya kilimo katika nchi hizo za Kiafrika.  Amesema kuwa, Benki ya Dunia imeamua kutoa misaada yake kwa nchi hizo kwa lengo la kustawisha zaidi utafiti katika sekta ya kilimo na kuboresha mafunzo kwenye sekta hiyo.

No comments:

Post a Comment