Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, March 20, 2013

Rwanda yawanyima viza wataalamu wa UN


Rwanda yawanyima viza wataalamu wa UN
Rwanda imekataa kutoa viza kwa maafisa wawili wa timu ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa iliyoituhumu Kigali mwaka jana kuwa inawapa silaha waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuwataja kuwa watu wenye upendeleo.
Mwanadiplomasia wa Rwanda amethibitisha hatua ya nchi hiyo ya kukataa kuwapa viza wataalamu hao wa Umoja wa Mataifa kwa jina la Bernad Leloup wa Ubelgiji na Marie Plamadiala wa Moldova. Kundi la wataalamu wa uchunguzi kutoka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linalosimamia utekelezaji wa vikwazo vya silaha na vingine dhidi ya Kongo lilisema katika ripoti yake ya mwaka jana kuwa Waziri wa Ulinzi wa Rwanda alikuwa akiamuru uasi wa kundi la M23 huko Congo na kwamba Rwanda pia ilikuwa ikiwapa silaha waasi wa kundi hilo sambamba na kuwasaidia wanajeshi wa kushirikiana nao katika mapigano. Kundi la wataalamu la uchunguzi kutoka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliituhumu pia Uganda kuwa inawaunga mkono waasi wa Machi 23. Rwanda na Uganda zote zimekanusha tuhuma hizo dhidi yao.

No comments:

Post a Comment