Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, March 18, 2013

Hatari zilizosalia baada ya kukaliwa kwa mabavu Iraq

Hatari zilizosalia baada ya kukaliwa kwa mabavu Iraq Wataalamu wa mashirika ya afya wameripoti kuwa athari zilioachwa huko Iraq baada ya uvamizi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya nchi hiyo ni hatari kwa vizazi vijavyo vya nchi hiyo.
Wataalamu wa mambo na mashirika ya afya ya Iraq yametahadharisha kuhusu hatari za athari mbaya za uvamizi na kukaliwa kwa mabavu Iraq na vikosi vya Marekani na kueleza kuwa Marekani ilitumia tani 35 za urani katika vita huko Iraq suala linalotishia maisha ya vizazi vijavyo. Munthi Mahmoud Shukr mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Baghdad ameashiria athari haribifu za urani kwa raia na mazingira ya maeneo yaliyoathiriwa na kueleza kuwa Marekani iliwatumia raia wa Iraq kama mapanya wa maabara na majaribio yake mbalimbali.

No comments:

Post a Comment