Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, March 9, 2013

Kamanda wa Kutuliza Ghasia Misri atimuliwa kazi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri Meja Jenerali Muhammad Ibrahim al Juma'a
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri amemtimua kazi Meja Jenerali Majid Nouh Kamanda wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia nchini humo. Meja Jenerali Muhammad Ibrahim al Juma'a amemtimua kazi Meja Jenerali Majid Nouh na badala yake amemteua Meja Jenerali Ashraf Abdullah kuziba nafasi hiyo. Siku ya Alhamisi iliyopita, mamia ya polisi wa Misri walifanya mgomo na kutaka  aondolewe Waziri wa Mambo ya Ndani  wa nchi hiyo. Polisi wa Misri wanamtuhumu waziri  huyo kuwa alitumia kikosi cha usalama kwa shabaha ya kufikia  malengo yake ya kisiasa. Kwa upande mwengine, jeshi la polisi katika mji wa Port Said nchini Misri limekabidhi ulinzi wa usalama wa mji huo kwa jeshi la nchi hiyo ili kukabiliana na ghasia na machafuko ya barabarani yanayoendelea mjini humo kwa siku kadhaa sasa.

No comments:

Post a Comment