Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, March 9, 2013

Yemen yaiomba radhi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Yemen yaiomba radhi Jamhuri ya Kiislamu ya IranWizara ya Mambo ya Ndani ya Yemn imeiomba radhi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kutoa taarifa za uwongo kwamba, Yemen imekamata meli ya Kiirani iliyokuwa imebeba shehena kubwa ya silaha. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Yemen imesema kuwa, inasikitishwa  na inakadhibisha taarifa zilizotangazwa nchini humo  juu ya kukamatwa  meli ya Kiirani iliyokuwa imesheheni silaha. Inafaa kuashiria hapa kuwa, tarehe 2 Februari mwaka 2013, serikali ya Yemen ilidai kwamba meli moja ya Kiirani imekamatwa kwenye bandari ya Mukala nchini humo ikiwa imebeba shehena kubwa ya silaha.

No comments:

Post a Comment