
Musyoka amewataka wafuasi wao kuwa watulivu na kusisitiza kwamba, CORD haina lengo la kuitisha maandamano ya kitaifa. Amesema viongozi wakuu wa muungano huo wanaendelea kujadiliana na huenda wakafika mahakamani kuwasilisha kilio chao. Hata hivyo mwenyekiti wa IEBC amewaambia wanahabari kwamba zoezi la kuhesabu kura litaendelea kwa kuwa hakuna sharia zilizokiukwa. Amekanusha tuhuma kwamba tume yake inashinikizwa na nchi za Magharibi kumtangaza mgombea fulani kuwa mshindi wa kiti cha urais. Hii ni katika hali ambayo, mgombea wa urais kwa tiketi ya muungano wa Jubilee, Uhuru Kenyatta anaendelea kuongoza hadi sasa baada ya takriban asilimia 40 ya kura zote kuhesabiwa na kutangazwa.
No comments:
Post a Comment