Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, March 19, 2013

Boko Haram waua walimu watatu Nigeria


Wanamgambo wa Boko Haram wakiwa wamejizatiti kwa silaha NigeriaWalimu watatu wameuawa katika mashambulio yaliyofanywa na watu wenye silaha dhidi ya shule mbili huko kaskazini mashariki mwa Nigeria. Walimu hao waliuawa jana katika mashambulio mawili yaliyotekelezwa na watu wenye silaha wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa kundi la Boko Haram katika mji wa Maiduguri unaopatikana katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Aidha wanafunzi kadhaa walijeruhiwa katika mashambulizi hayo. Kabla ya hapo pia, watu 25 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kutokea milipuko mitano katika mji wa Kano kaskazini mwa Nigeria. Hadi sasa hakuna mtu au kundi lolote lililotangaza kuhusika na mashambulio hayo, lakini kundi la Boko Haram linashukiwa kuwa ndilo lililotekeleza mashambulio hayo kwa vile limekuwa likitekeleza mashambulio kama hayo katika maeneo tofauti ya nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika.

No comments:

Post a Comment