Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, March 19, 2013

Mapigano kati ya jeshi na waasi Sudan Kusini


Waasi wenye silaha nchini Sudan KusiniShirika la Msalaba Mwekundu limetangaza kuwa, zaidi ya watu 60 wamejeruhiwa katika mapigano ya hivi karibuni kati ya jeshi la Sudan Kusini na kundi moja la waasi nchini humo. Shirika hilo limeongeza kuwa, katika kipindi cha wiki mbili zilizopita karibu watu 62 waliojeruhiwa katika apigano hayo walitibiwa katika kituo kimoja cha afya cha shirika hilo na kwamba. Mmoja wa viongozi wandamizi wa shirika hilo amenukuliwa akisema kuwa, idadi rasmi ya maafa yaliyotokana na machafuko hayo ya pande mbili haijafahamika kutokana na kwamba, hadi sasa hakuna taasisi yoyote iliyofika eneo la tukio na kufanya uchunguzi. Ameongeza kuwa, kutokana na viongozi wa Juba kukosa ripoti kamili ya mapigano hayo, idadi ya wahanga inaweza kupindukia ile iliyotajwa hapo awali. Hivi karibuni mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, alielezea kusikitishwa kwake na vitendo vya kikatili vinavyofanywa na Jeshi la Sudan Kusini dhidi ya waasi wanaoongozwa na David Yauyauambao wanaipinga serikali ya Juba.

No comments:

Post a Comment