Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, March 9, 2013

Mamilioni walalamikia marufuku ya hijabu Uturuki


Mamilioni walalamikia marufuku ya hijabu Uturuki
Zaidi ya watu milioni 12 wametaka iondoshwe marufuku ya hijabu nchini Uturuki. Mkuu wa Vyama vya Wafanyakazi  Serikalini  nchini Uturuki amesema kuwa, jumla ya watu milioni 12 wanapinga kuendelezwa marufuku ya hijabu  mashuleni  na hata kunyimwa  ajira wanawake wanaovaa hijabu kwenye sekta za serikali nchini humo. Mkuu wa Vyama vya Wafanyakazi Serikalini nchini Uturuki  amewasilisha ombi hilo kwa Waziri wa Kazi na Ustawi wa Jamii wa Uturuki jumla ya saini za watu milioni 12 wanaotaka kuondoshwa marufuku ya hijabu nchini humo. Waziri wa Kazi na Ustawi wa Jamii wa Uturuki ameahidi kulipeleka ombi hilo mbele ya kikao cha baraza la mawaziri nchini humo ili lijadiliwe upya.

No comments:

Post a Comment