Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, March 19, 2013

Wazimbabwe waipigia kura ya ndio katiba mpya


Wazimbabwe waipigia kura ya ndio katiba mpya
Matokeo yasiyo rasmi ya kura ya maoni ya katiba mpya nchini Zimbabwe, yanaonyesha kwamba, wananchi wameipigia kura ya ndio katiba hiyo ambayo inapunguza madaraka ya rais wa baadaye wa nchi hiyo. Ripoti zilizosambazwa leo kutoka vituo vya kuhesabu kura, zinaonyesha kuwa, watu milioni tatu na laki moja kati ya watu milioni tatu na laki nne waliofika kwenye vituo vya kupigia kura nchini humo, wameipigia kura ya ndio katiba mpya ya nchi hiyo ya kusini mwa Afrika inayokabiliwa na mgogoro mkubwa wa kiuchumi. Gazeti la Herald limeripoti kuwa, watu laki mbili wameipigia kura ya hapana katiba hiyo. Kwa mujibu wa takwimu rasmi za nchi hiyo, Wazimbabwe milioni sita pekee ndio waliokamilisha masharti ya kupiga kura nchini. Ilitarajiwa kuwa, hadi kufikia jioni ya leo, Tume ya Uchaguzi nchini humo ingekuwa imekamilisha kazi za kuhesabu kura na kutangaza matokeo rasmi ya kura hiyo.

No comments:

Post a Comment