Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, March 18, 2013

Watu 10 wauawa kwenye mlipuko nchini Somalia


Watu 10 wauawa kwenye mlipuko nchini Somalia
Habari kutoka Mogadishu, mji mkuu wa Somalia zinasema kuwa, kwa akali watu 10 wamefariki dunia na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mlipuko mkubwa wa bomu uliotokea karibu na ukumbi wa kitaifa wa michezo ya kuigiza.
Habari zaidi zinasema kuwa, bomu hilo lilikuwa limetegwa kwenye gari na kwamba Mkuu wa Usalama wa Mogadishu ndiye alikuwa mlengwa mkuu. Haijabainika wazi iwapo mkuu huyo ameuawa au la.
Kundi la wanamgambo la Al-shabab tayari limedai kuhusika na shambulio hilo. Kundi hilo limeapa kumuondoa madarakani Rais Hassan Sheikh Mohamud, aliyechaguliwa na bunge la Somalia mwaka uliopita. Hii ni katika hali ambayo, wanamgambo hao wanaripotiwa kuuteka mji wa Hudur wa kusini mwa Somalia.

No comments:

Post a Comment