| Hivi
 ndivyo hali ilivyokuwa kwenye mtaa wa Kariakoo jijini Dar es Salaam 
ambapo askari na watu wachache wanaonekana jirani na jengo la 
DDC-Kariakoo, (Kushoto), baada ya hofu ya kuwepo kwa maandamano baada ya
 sala ya Ijumaa jana Novemba 2, 2012. Shughuli za kibiashara 
zilitatizika kwa muda wa masaa matatu baada ya sala ya Ijumaa, ambapo 
kikundi cha watu wachache wanaoaminika kuwa ni wafuasi wa Sheikh Ponda 
Issa Ponda, kilionekana kikiwa nje ya msikiti wa Idrisa baada ya sala 
hiyo. Hata hivyo polisi baada ya kuwaeleza mara kadhaa kutawanyika na 
kutofanya hivyo, ilirusha mabomu ya machozi na kupiga risasi hewani ili 
kuwatawanya hali iliyozusha hofu kuu miongoni mwa wapita njia na wafanyabiashara na kupelekea kufunga maduka yao kwa muda.
 Sheikh Ponda na wenzake 49 wanakabilkiwa na kesi ya kuvamia eneo la 
Markaz, Chang'ombe jijini ambapo pamoja na mambo mengine, wanatuhumiwa 
kuvunja na kuiba pamoja na kujimilikisha ardhi kinyume cha sheria. 
Washtakiwa wote walikubaliwa dhamana juzi Alhamisi Novemba 1, 2012 
isipokuwa sheikh Ponda ambaye bado Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) 
hajaondoa pingamizi lake la kuzuia dhamana. Kwa waliopewa dhamana, 
masharti ni kuwa na wadhamini wawili na kuweka bondi ahadi ya shilingi 
milioni moja kila mmoja, pamoja na barua ya kuonyesha anuani maalum ya 
makazi. Sharti lingine kwa mujibu wa hakimu ......................ni 
washtakiwa kutokanyaga eneo la Markaz hadi hapo kesi yao 
itakapokamilika. Bado haijajulikana kama washtakiwa wote wametimiza 
masharti ya dhamana. | 
No comments:
Post a Comment