Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 18, 2012

Wananchi wa Sierra Leone washiriki uchaguzi mkuu



Wananchi wa Sierra Leone washiriki uchaguzi mkuu
Mamilioni ya raia nchini Sierra Leone, wameelekea kwenye masanduku ya kupigia kura Jumamosi hii ili kumchagua rais na wabunge wapya. Hali imekuwa shwari katika vituo vingi vya upigaji kura hususan mji mkuu, Freetown. Rais wa sasa, Ernest Bai Koroma anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa wagombea wengine 8 wa kiti cha rais. Hata hivyo weledi wa mambo wanaamini kuwa mchuano mkali utakuwa kati ya Rais Bai na mpinzani wake wa karibu, Julius Maada Bio anayewania wadhifa huo kwa tiketi ya chama cha Sierra Leone Peoples Party (SLPP). Bai Koroma alichaguliwa kuwa rais mwaka 2007 na anapania kutetea wadhifa wake kwa kipindi kingine cha pili. Sierra Leone imekumbwa na vita vya ndani kwa muda mrefu na ni miongoni mwa nchi masikini zaidi duniani licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa madini ya almasi.

No comments:

Post a Comment