skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
Wimbi la mashambulio ya kigaidi nchini Iraq
      
    
  
  
  
   
   
   
   
      
   
    
     
    
    
    
    
   
   
     Jumanne tarehe 27 Novemba ilikuwa siku ya umwagaji damu mkubwa 
kwa Iraq na Wairaqi. Milipuko minane iliitikisa miji mbalimbali ya ya 
nchi hiyo na kwa akali watu 29 walipoteza maisha yao na zaidi ya mia 
moja na ishirini kujeruhiwa. Miji ya Kirkuk, Al Anbar na Baghdad ndiyo 
iliyolengwa na magaidi hapo jana. Polisi ya Iraq imelinyooshea kidole 
cha tuhuma kundi la mtandao wa al-Qaeda. Hata hivyo al-Qaeda ambalo ni 
kundi lililolelewa na Marekani, ni moja tu kati ya makumi ya makundi ya 
kigaidi ambayo yanaendesha harakati zao nchini Iraq. Inapaswa pia 
kuongeza katika majimui hiyo, harakati za kisiasa zinazoipinga serikali 
ya Baghdad na Noury al-Maliki mwenyewe, Waziri Mkuu wa nchi hiyo. 
Ushirikiano wa makundi na harakati hizi za kisiasa na magaidi, hadi sasa
 umeandaa uwanja wa kutokea milipuko na operesheni kadhaa za kigaidi 
nchini humo. Ni jambo linaloeleweka wazi kuwa, mrengo wa al-Iraqiya 
unaoongozwa na Iyad Allawi, una uhusiano wa karibu na makundi amilifu ya
 kigaidi nchini Iraq. Nchi kama Saudi Arabia, Qatar na Jordan ambazo 
hazifurahishwi na muundo wa kisiasa wa Iraq na hata Waziri Mkuu Noury 
al-Maliki, daima zimekuwa zikiuunga mkono mrengo wa al-Iraqiya na 
makundi amilifu ya kigaidi katika nchi hiyo na kuyapatia misaada ya kila
 upande. Nchi hizo, zimekuwa zikiutumia mrengo huo kama wenzo wa 
mashinikizo dhidi ya al-Maliki na ikilazimu walitumie kundi hilo kutoa 
pigo kwa serikali ya Baghdad na hivyo kuutilia alama ya swali utendaji 
wa al-Maliki. Hadi sasa makumi ya magaidi ambao ni raia wa Saudia, 
Imarati na Jordan wametiwa mbaroni. Huu ni ushahidi kwamba, Iraq 
inakabiliwa na njama kali pia kutoka kwa baadhi ya nchi za Kiarabu. 
   Nchi hizi za Kiarabu ambazo aghlabu zina uhusiano baridi na Iraq 
daima zimekuwa zikihesabiwa kuwa tishio kwa uthabiti wa kisiasa na 
kiusalama wa nchi hiyo. Pamoja na hayo, akthari ya weledi wa masuala ya 
kisiasa wanaamini kwamba, kuibuka wimbi jipya la machafuko huko Iraq 
bila shaka kutakuwa na uhusiano wa namna fulani na matukio ya Mashariki 
ya Kati yakiwemo ya Syria. Jumanne ya jana magari manane yaliyotegwa 
mabomu ndani yake yaliripuka katika miji mbalimbali ya nchi hiyo. Syria 
nayo ilikuwa na hali kama hiyo hiyo. Hii inaonesha kuwa, kuna njama za 
pamoja ambazo zinatekelezwa dhidi ya nchi hizo. Inaonekana kuwa, mamluki
 wa nchi za Kiarabu na makundi ya kigaidi ambayo yanapatiwa misaada ya 
kifedha na silaha na mhimili wa pamoja wa Kimagharibi-Kiarabu ulio dhidi
 ya Syria unataka kuishughulisha Iraq na Syria kwa migogoro ili uweze 
kunufaika na anga hiyo kwa maslahi yake. Iraq ni miongoni mwa nchi za 
eneo la Mashariki ya Kati ambazo hadi sasa zimekataa kuungana na mhimili
 ulio dhidi ya Syria.  Hapana shaka kuwa, jambo hilo limeikasirisha mno 
Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu ambazo ziko pamoja na Washington 
katika kadhia ya Syria. Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kuwa,
 moja ya sababu za kuzusha machafuko na sokomoko nchini Iraq ni kutaka 
kuilazimisha nchi hiyo ikubaliane na matakwa ya nchi za Magharibi 
kuhusiana na migogoro ya Mashariki ya Kati.
Jumanne tarehe 27 Novemba ilikuwa siku ya umwagaji damu mkubwa 
kwa Iraq na Wairaqi. Milipuko minane iliitikisa miji mbalimbali ya ya 
nchi hiyo na kwa akali watu 29 walipoteza maisha yao na zaidi ya mia 
moja na ishirini kujeruhiwa. Miji ya Kirkuk, Al Anbar na Baghdad ndiyo 
iliyolengwa na magaidi hapo jana. Polisi ya Iraq imelinyooshea kidole 
cha tuhuma kundi la mtandao wa al-Qaeda. Hata hivyo al-Qaeda ambalo ni 
kundi lililolelewa na Marekani, ni moja tu kati ya makumi ya makundi ya 
kigaidi ambayo yanaendesha harakati zao nchini Iraq. Inapaswa pia 
kuongeza katika majimui hiyo, harakati za kisiasa zinazoipinga serikali 
ya Baghdad na Noury al-Maliki mwenyewe, Waziri Mkuu wa nchi hiyo. 
Ushirikiano wa makundi na harakati hizi za kisiasa na magaidi, hadi sasa
 umeandaa uwanja wa kutokea milipuko na operesheni kadhaa za kigaidi 
nchini humo. Ni jambo linaloeleweka wazi kuwa, mrengo wa al-Iraqiya 
unaoongozwa na Iyad Allawi, una uhusiano wa karibu na makundi amilifu ya
 kigaidi nchini Iraq. Nchi kama Saudi Arabia, Qatar na Jordan ambazo 
hazifurahishwi na muundo wa kisiasa wa Iraq na hata Waziri Mkuu Noury 
al-Maliki, daima zimekuwa zikiuunga mkono mrengo wa al-Iraqiya na 
makundi amilifu ya kigaidi katika nchi hiyo na kuyapatia misaada ya kila
 upande. Nchi hizo, zimekuwa zikiutumia mrengo huo kama wenzo wa 
mashinikizo dhidi ya al-Maliki na ikilazimu walitumie kundi hilo kutoa 
pigo kwa serikali ya Baghdad na hivyo kuutilia alama ya swali utendaji 
wa al-Maliki. Hadi sasa makumi ya magaidi ambao ni raia wa Saudia, 
Imarati na Jordan wametiwa mbaroni. Huu ni ushahidi kwamba, Iraq 
inakabiliwa na njama kali pia kutoka kwa baadhi ya nchi za Kiarabu. 
   Nchi hizi za Kiarabu ambazo aghlabu zina uhusiano baridi na Iraq 
daima zimekuwa zikihesabiwa kuwa tishio kwa uthabiti wa kisiasa na 
kiusalama wa nchi hiyo. Pamoja na hayo, akthari ya weledi wa masuala ya 
kisiasa wanaamini kwamba, kuibuka wimbi jipya la machafuko huko Iraq 
bila shaka kutakuwa na uhusiano wa namna fulani na matukio ya Mashariki 
ya Kati yakiwemo ya Syria. Jumanne ya jana magari manane yaliyotegwa 
mabomu ndani yake yaliripuka katika miji mbalimbali ya nchi hiyo. Syria 
nayo ilikuwa na hali kama hiyo hiyo. Hii inaonesha kuwa, kuna njama za 
pamoja ambazo zinatekelezwa dhidi ya nchi hizo. Inaonekana kuwa, mamluki
 wa nchi za Kiarabu na makundi ya kigaidi ambayo yanapatiwa misaada ya 
kifedha na silaha na mhimili wa pamoja wa Kimagharibi-Kiarabu ulio dhidi
 ya Syria unataka kuishughulisha Iraq na Syria kwa migogoro ili uweze 
kunufaika na anga hiyo kwa maslahi yake. Iraq ni miongoni mwa nchi za 
eneo la Mashariki ya Kati ambazo hadi sasa zimekataa kuungana na mhimili
 ulio dhidi ya Syria.  Hapana shaka kuwa, jambo hilo limeikasirisha mno 
Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu ambazo ziko pamoja na Washington 
katika kadhia ya Syria. Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kuwa,
 moja ya sababu za kuzusha machafuko na sokomoko nchini Iraq ni kutaka 
kuilazimisha nchi hiyo ikubaliane na matakwa ya nchi za Magharibi 
kuhusiana na migogoro ya Mashariki ya Kati.
    
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment