Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 6, 2012

Wapalestina kutetea haki yao Umoja wa Mataifa



Wapalestina  kutetea haki yao Umoja wa MataifaMamlaka ya Ndani ya Palestina imepuuzilia mbali vitisho vya Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel Benjamin Netanyahu na kusisitiza kwamba itasonga mbele na mipango ya kuutaka Umoja wa Mataifa uitambue rasmi Palestina kama mwanachama kamili.
Hapo Jana Netanyahu alimpigia simu Rais wa mamlaka ya ndani ya Palestina, Mahmoud Abbas akimtaka kutokwenda Umoja wa Mataifa na badala yake arudi kwenye meza ya mazungumzo na Wazayuni. Netanyahu ametishia kwamba endapo Abbas ataenda Umoja wa Mataifa, mazungumzo eti ya amani yatakosa maana na kwamba Wapalestina watakabiliwa na mashinikizo zaidi.
Palestina ikipata uanachama kamili itakuwa na uwezo wa kuiburuza Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) jambo ambalo Tel Aviv inaliogopa mno.

No comments:

Post a Comment