
Msemaji wa polisi ya Msumbuji Pedro Cossa amesema Dhlakama si mtoto mdogo na kwa msingi huo serikali inaamini kwamba hatatekeleza vitisho vya kuanzisha tena vita vya ndani nchini. Amesisitiza kuwa Afonso Dhlakama ameahidi mara nyingi kwamba hataanzisha tena vita vya ndani na inatarajiwa kwamba hatabadili msimamo wake.
Kiongozi wa waasi wa zamani wa Msumbiji ametishia kuwa ataanzisha tena wimbi la damu nchini humo iwapo serikali haitagawa utajiri unaoongezeka kila kwa watu wote na kufanyia marekebisho mfumo wa uchaguzi.
No comments:
Post a Comment