Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 15, 2012

'Mashambulio ya Israel hayatadhoofisha irada ya Gaza'

'Mashambulio ya Israel hayatadhoofisha irada ya Gaza' Waziri Mkuu wa serikali halali ya Palestina huko Ghaza amesema kuwa wakazi wa Ukanda wa Ghaza wako tayari kukabiliana na mashambulizi ya jeshi la utawala haramu wa Kizayuni. Ismail Hania amesema kuwa kushadidi mashambulizi ya utawala ghasibu wa Kizayuni huko Ghaza hakutadhoofisha azma na irada ya wakazi wa eneo hilo.
Hania ameyasema hayo baada ya kuwatembelea katika hospitali ya al Shifaa baadhi ya Wapalestina waliojeruhiwa katika mashambulio ya hivi karibuni ya jeshi la Israel huko Ukanda wa Ghaza. Hania ameongeza kuwa serikali halali ya Palestina imeanzisha harakati kadhaa katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kidiplomasia kupitia kuwasiliana na viongozi wa nchi za Kiarabu na pia taasisi za kieneo na kimataifa ili kusaidia kudhibiti mashambulizi ya utawala ghasibu wa Kizayuni huko Ghaza. Waziri Mkuu wa serikali halali ya Palestina huko Ghaza amesema wameziomba pande za Kiarabu na kimataifa kuwashtaki na kuwahukumu viongozi wote wa utawala ghasibu wa Israel waliohusika na jinai chungu nzima dhidi ya raia wa Kipalestina wa Ukanda wa Ghaza.

No comments:

Post a Comment