skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
'Mashambulio ya Israel hayatadhoofisha irada ya Gaza' 
    
     
    
    
    
    
   
    
 Waziri Mkuu wa serikali halali ya 
Palestina huko Ghaza amesema kuwa wakazi wa Ukanda wa Ghaza wako tayari 
kukabiliana na mashambulizi ya jeshi la utawala haramu wa Kizayuni. 
Ismail Hania amesema kuwa kushadidi mashambulizi ya utawala ghasibu wa 
Kizayuni huko Ghaza hakutadhoofisha azma na irada ya wakazi wa eneo 
hilo.
Waziri Mkuu wa serikali halali ya 
Palestina huko Ghaza amesema kuwa wakazi wa Ukanda wa Ghaza wako tayari 
kukabiliana na mashambulizi ya jeshi la utawala haramu wa Kizayuni. 
Ismail Hania amesema kuwa kushadidi mashambulizi ya utawala ghasibu wa 
Kizayuni huko Ghaza hakutadhoofisha azma na irada ya wakazi wa eneo 
hilo.  
Hania ameyasema hayo baada ya kuwatembelea katika hospitali ya al 
Shifaa baadhi ya Wapalestina waliojeruhiwa katika mashambulio ya hivi 
karibuni ya jeshi la Israel huko Ukanda wa Ghaza. Hania ameongeza kuwa 
serikali halali ya Palestina imeanzisha harakati kadhaa katika nyanja 
mbalimbali zikiwemo za kidiplomasia kupitia kuwasiliana na viongozi wa 
nchi za Kiarabu na pia taasisi za kieneo na kimataifa ili kusaidia 
kudhibiti mashambulizi ya utawala ghasibu wa Kizayuni huko Ghaza. Waziri
 Mkuu wa serikali halali ya Palestina huko Ghaza amesema wameziomba 
pande za Kiarabu na kimataifa kuwashtaki na kuwahukumu viongozi wote wa 
utawala ghasibu wa Israel waliohusika na jinai chungu nzima dhidi ya 
raia wa Kipalestina wa Ukanda wa Ghaza.
    
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment