Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 14, 2012

UN yataka kusitishwa machafuko Myanmar



UN yataka kusitishwa machafuko Myanmar
Umoja wa Mataifa umeitaka serikali ya Myanmar kusitisha mara moja machafuko nchini humo. Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kutiwa wasiwasi na kuendelea machafuko huko Myanmar na kuitaka serikali ya nchi hiyo kukomesha haraka iwezekanavyo mashambulizi dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo. Martin Nisirky msemaji wa Ban Ki Moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameashiria hali ngumu inayowakabili wakimbizi wa Kiislamu wa Myanmar na kueleza kuwa Umoja wa Mataifa unaitaka serikali ya nchi hiyo kusitisha mara moja mashambulizi dhidi ya Waislamu na kuzingatia hali ya Waislamu wa nchi hiyo. Nisirky amesema hali ni ya kutia wasiwasi huko katika mkoa wa Rakhine na maelfu ya watu wameamua kuukimbia mkoa huo kupitia njia ya majini na kwamba wamepata ripoti mbaya kuhusu hali za watu hao.

No comments:

Post a Comment