Harakati ya Jihadul Islami ya 
Palestina imesema kuwa, kuna udharura wa Misri kusimamia utekelezwaji wa
 makubaliano ya maridhiano ya kitaifa kati ya makundi ya Palestina. 
Khalid al Batwash afisa mwandamizi wa harakati ya Jihadul Islami ya 
Palestina amesema hayo leo alipokutana na maulamaa wa Misri katika 
Ukanda wa Gaza na kuwataka viongozi wa Cairo kupatanisha katika suala la
 utekelezaji makubaliano ya maridhiano ya kitaifa kati ya harakati ya 
Fat'h na Hamas.
Amesisitiza kuwa, kuendelea hitilafu 
kati ya makundi ya Palestina ni kwa manufaa ya adui Mzayuni. Viongozi wa
 harakati hizo mbili za Palestina Februari 5 mwaka huu walitia saini 
mjini Doha, Qatar makubaliano ya kuweka kando hitilafu zao kwa lengo la 
kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na kuitisha uchaguzi, lakini hadi 
sasa makubaliano hayo bado hayajatekelezwa.







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment