Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, November 10, 2012

Misri yatakiwa kusimamia maridhiano ya Palestina

Misri yatakiwa kusimamia maridhiano ya Palestina
Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina imesema kuwa, kuna udharura wa Misri kusimamia utekelezwaji wa makubaliano ya maridhiano ya kitaifa kati ya makundi ya Palestina. Khalid al Batwash afisa mwandamizi wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amesema hayo leo alipokutana na maulamaa wa Misri katika Ukanda wa Gaza na kuwataka viongozi wa Cairo kupatanisha katika suala la utekelezaji makubaliano ya maridhiano ya kitaifa kati ya harakati ya Fat'h na Hamas.

Amesisitiza kuwa, kuendelea hitilafu kati ya makundi ya Palestina ni kwa manufaa ya adui Mzayuni. Viongozi wa harakati hizo mbili za Palestina Februari 5 mwaka huu walitia saini mjini Doha, Qatar makubaliano ya kuweka kando hitilafu zao kwa lengo la kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na kuitisha uchaguzi, lakini hadi sasa makubaliano hayo bado hayajatekelezwa.

No comments:

Post a Comment