Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, November 26, 2012

UN: Unyanyasaji dhidi ya wanawake ukomeshwe



UN: Unyanyasaji dhidi ya wanawake ukomeshwe
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kukomeshwa vitendo vya utumiaji mabavu na kuwanyanyasa wanawake. Ban Ki Moon amesema hayo katika risala yake kwa mnasaba wa Novemba 25, Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Unyanyasaji wa Wanawake. Ban Ki Moon amesema, licha ya kuweko hatua zilizochukuliwa za kupambana na unyanyasaji dhidi ya wanawake, asilimia 70 ya wanawake hukabiliwa na vitendo vya utumiaji mabavu na unyanyasaji wa kijinsia katika kipindi cha maisha yao na kwamba, robo ya wanawake huwa ni wajawazito. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema, utumiaji mabavu dhidi ya wanawake ni misdaqi ya wazi ya ukiukaji wa haki za binadamu na kwamba, nchi zanachama za umoja huo zinapaswa kuandaa mipango na mikakati ya kung'oa mizizi ya vitendo hivyo vibaya.

No comments:

Post a Comment