Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kukomeshwa vitendo
 vya utumiaji mabavu na kuwanyanyasa wanawake. Ban Ki Moon amesema hayo 
katika risala yake kwa mnasaba wa Novemba 25, Siku ya Kimataifa ya 
Kupambana na Unyanyasaji wa Wanawake. Ban Ki Moon amesema, licha ya 
kuweko hatua zilizochukuliwa za kupambana na unyanyasaji dhidi ya 
wanawake, asilimia 70 ya wanawake hukabiliwa na vitendo vya utumiaji 
mabavu na unyanyasaji wa kijinsia katika kipindi cha maisha yao na 
kwamba, robo ya wanawake huwa ni wajawazito. Katibu Mkuu wa Umoja wa 
Mataifa amesema, utumiaji mabavu dhidi ya wanawake ni misdaqi ya wazi ya
 ukiukaji wa haki za binadamu na kwamba, nchi zanachama za umoja huo 
zinapaswa kuandaa mipango na mikakati ya kung'oa mizizi ya vitendo hivyo
 vibaya.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment