Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, November 30, 2012

Vikwazo vya Marekani dhidi ya vyombo vya habari Iran



Vikwazo vya Marekani dhidi ya vyombo vya habari IranBaraza la Seneti la Marekani liko katika mikakati ya kuweka vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ikiwemo kuzuia fedha zote zinazofungamana na Taasisi ya Redio na Televisheni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB. Taarifa zinasema kuwa, vikwazo hivyo vipya vya Marekani dhidi ya IRIB ni mwendelezo wa njama za nchi za Magharibi na hasa Marekani za kuvinyamazisha vyombo vya habari vya hapa nchini. Taarifa hiyo imeeleza kuwa,
mkakati huo  wa Seneti ya Marekani pamoja na hatua za hivi karibuni za wakuu wa Eutelsat  na Intelsat za kukataa kurusha kupitia satalaiti zao vipindi vya kanali mbalimbali za televisheni na redio za Iran mwezi uliopita, ni ukiukaji wa wazi wa uhuru wa kujieleza na kupasha habari. Kusitishwa urushwaji wa matangazo hayo kwenye satalaiti hizo kulitokana na mashinikizo ya wakuu wa nchi za Umoja wa Ulaya. Mwanzoni mwa mwezi huu, satalaiti ya Asiasat iliyoko Hong Kong nayo pia ilisimamisha kurusha hewani matangazo ya redio na televisheni za Iran kutokana na mashinikizo ya Marekani. Hali kadhalika, Marekani imeshaiwekea vikwazo Iran katika sekta za mafuta, nishati, bandari na mashirika ya meli. Mwendelezo wa vikwazo vya nchi za Magharibi na hasa Marekani dhidi ya Iran unatokana na madai yao potofu kwamba Iran ina mpango wa kutengeneza mabomu ya nyuklia, amma viongozi wa Tehran na hata Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia IAEA wamesisitiza mara kadhaa kwamba mpango wa nyuklia wa Iran unafanyika kwa malengo ya amani tena chini ya usimamizi wa wakaguzi wa IAEA. 

No comments:

Post a Comment