 
 
Dk. Juma Salum Mambi ambae ni Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, akifafanua jambo  kwa wajumbe kuhusu katiba yao
.………………………………………………………
Na Fatma Mzee, Maelzeo
JUMUIYA ya Madaktari 
Zanzibar, imefanya mkutano wa kujadili katiba yake kwa lengo la 
kuifanyia marekebisho ili iende na wakati wa sasa. 
 Miongoni mwa marekebisho hayo, ni pamoja na kuongeza kipengele cha jumuiya hiyo kuwa na  mwanasheria wake.
 Mwenyekiti wa jumuiya
 hiyo ambaye ndiye aliyeongoza mkutano huo Dk. Said Mohamed Abdullah, 
aliwashauri wanachama kuisoma vyema katiba hiyo na kuainisha maeneo 
wanayohisi yanahitaji kurekebishwa ili kuiimarisha zaidi .
 Alisisitiza
 umuhimu kwa wanachama kutopuuza kuhudhuria na kufuatilia vikao kwa 
lengo la kuwa na jumuiya iliyo imara na inaweza kusimamia vizuri 
matarajio yao.
 Hata
 hivyo, wajumbe wote wa jumuiya hiyo walikubaliana na katiba hiyo, 
ingawa baadhi yao waliomba wapatiwe muda zaidi wa kuipitia kwa kina 
kabla kutoa mapendekezo yao.
 Mjumbe
 mmoja Yussuf Haji, aliwaomba wanachama wenzake kuiheshimu katiba hiyo, 
kwani ndio muongozo utakaowezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. 
 Kwa
 upande wake, Katibu wa jumuiya hiyo Dk. Juma Salum Mambi alisema, ili 
jumuiya hiyo ifanikiwe na na kufanana na jumuiya nyengine zilizopiga 
hatua kubwa, ni vyema madaktari wazingatie haja ya kuzidi kuonesha umoja
 na mshikamano utakaosaidia kuiimarisha jumuiya yao.
 Mkutano huo umeakhirishwa hadi Disemba 8, mwaka huu ili kutoa fursa kwa wanachama kuipitia kikamilifu katiba hiyo.







 
 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment