Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 25, 2012

Madaktari Zanzibar wakutana kuajadili katiba yao


 
Dk. Juma Salum Mambi ambae ni Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, akifafanua jambo  kwa wajumbe kuhusu katiba yao
.………………………………………………………
Na Fatma Mzee, Maelzeo
JUMUIYA ya Madaktari Zanzibar, imefanya mkutano wa kujadili katiba yake kwa lengo la kuifanyia marekebisho ili iende na wakati wa sasa.
 Miongoni mwa marekebisho hayo, ni pamoja na kuongeza kipengele cha jumuiya hiyo kuwa na  mwanasheria wake.
 Mwenyekiti wa jumuiya hiyo ambaye ndiye aliyeongoza mkutano huo Dk. Said Mohamed Abdullah, aliwashauri wanachama kuisoma vyema katiba hiyo na kuainisha maeneo wanayohisi yanahitaji kurekebishwa ili kuiimarisha zaidi .
 Alisisitiza umuhimu kwa wanachama kutopuuza kuhudhuria na kufuatilia vikao kwa lengo la kuwa na jumuiya iliyo imara na inaweza kusimamia vizuri matarajio yao.
 Hata hivyo, wajumbe wote wa jumuiya hiyo walikubaliana na katiba hiyo, ingawa baadhi yao waliomba wapatiwe muda zaidi wa kuipitia kwa kina kabla kutoa mapendekezo yao.
 Mjumbe mmoja Yussuf Haji, aliwaomba wanachama wenzake kuiheshimu katiba hiyo, kwani ndio muongozo utakaowezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
 Kwa upande wake, Katibu wa jumuiya hiyo Dk. Juma Salum Mambi alisema, ili jumuiya hiyo ifanikiwe na na kufanana na jumuiya nyengine zilizopiga hatua kubwa, ni vyema madaktari wazingatie haja ya kuzidi kuonesha umoja na mshikamano utakaosaidia kuiimarisha jumuiya yao.
 Mkutano huo umeakhirishwa hadi Disemba 8, mwaka huu ili kutoa fursa kwa wanachama kuipitia kikamilifu katiba hiyo.

No comments:

Post a Comment