Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 13, 2012

Polisi 29 wauawa kwenye mapigano nchini Kenya

Polisi  29 wauawa kwenye mapigano nchini Kenya
Askari polisi  wasiopungua 29 wameuawa nchini Kenya baada ya kutokea mapigano kati ya  watu wanaobeba silaha na askari polisi katika eneo la kaskazini mwa nchi hiyo. Tarifa zinasema kuwa, mapigano hayo yamejiri kati ya askari polisi na kundi la watu wanaobeba silaha katika wilaya ya Baragoi iliyoko kaskazini mwa Kenya na kupeleka askari polisi hao kuuawa na wengine zaidi ya 21 kujeruhiwa, wakiwa kwenye operesheni ya kutafuta ng'ombe. Jeshi la Polisi  nchini Kenya limethibitisha kuuawa askari polisi hao 29 katika shambulio hilo la watu wanaobeba silaha. Hayo yanahesabiwa kuwa ni mauaji makubwa zaidi kufanywa dhidi ya askari polisi tokea nchi hiyo ilipojinyakulia uhuru wake karibu miaka 50 iliyopita.

No comments:

Post a Comment