Askari polisi  wasiopungua 29 wameuawa nchini Kenya baada ya 
kutokea mapigano kati ya  watu wanaobeba silaha na askari polisi katika 
eneo la kaskazini mwa nchi hiyo. Tarifa zinasema kuwa, mapigano hayo 
yamejiri kati ya askari polisi na kundi la watu wanaobeba silaha katika 
wilaya ya Baragoi iliyoko kaskazini mwa Kenya na kupeleka askari polisi 
hao kuuawa na wengine zaidi ya 21 kujeruhiwa, wakiwa kwenye operesheni 
ya kutafuta ng'ombe. Jeshi la Polisi  nchini Kenya limethibitisha kuuawa
 askari polisi hao 29 katika shambulio hilo la watu wanaobeba silaha. 
Hayo yanahesabiwa kuwa ni mauaji makubwa zaidi kufanywa dhidi ya askari 
polisi tokea nchi hiyo ilipojinyakulia uhuru wake karibu miaka 50 
iliyopita.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment