Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 29, 2012

Waasi wa M23 wajitayarisha kuondoka Goma


Waasi wa M23 wajitayarisha kuondoka Goma
Waasi wa mashariki mwa Kongo DRC wamesema kuwa wanaanza kuondoka katika mji waliouteka wa Goma, ikiwa ni siku kadhaa baada kufikia makubaliano na serikali kwa upatanishi wa Uganda. Amani Kabashi msemaji wa waasi wa M23 amesema kuwa, wanaanza kundoka katika mji wa Masisi ulioko kilomita 50 kutoka katika jiji la Goma, kisha wataondoka katika eneo la Sake na mwishowe wataondoka kikamilifu katika mji wa Goma.  Hii ni katika hali ambayo Herve Ladsous, Mkuu wa askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Kongo amethibitisha kuwa waasi hao wameacha kusonga mbele na kwamba kuna dalili za kuondoka katika mji wa Goma. Wakati huo huo Jean Marie Runinga, kiongozi wa kisiasa wa waasi wa M23 amesema, kundi hilo halipingi kuondoka katika mji wa Goma, na kwamba bila ya shaka yoyote litafanya hivyo baada ya kutekelezwa masharti yake. Amesema, miongoni mwa masharti ya waasi hao ni kuachiliwa huru Etienne Tshisekedi, kiongozi wa upinzani aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Kongo. Tshisekedi anashikiliwa katika kifungo cha nyumbani tangu alipojitangazia ushindi baada ya uchaguzi wa rais wa mwaka uliopita  ambapo Rais Joseph Kabila alitangazwa mshindi.

No comments:

Post a Comment