Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 18, 2012

Tanzania na Malawi kutatua mgogoro wa Ziwa Nyasa



Tanzania na Malawi kutatua mgogoro wa Ziwa Nyasa
Serikali za Tanzania na Malawi zimefikia makubaliano ya kumtafuta mpatanishi wa kimataifa atakayetatua hitilafu za mpaka wa majini kati ya nchi hizo mbili. Bernard Membe Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania ameyasema hayo mjini Dar es Salaam alipokutana na mwenzake Ephrahim Muganda Chiume wa Malawi na kuongeza kuwa, pande hizo mbili zimechukua uamuzi wa pamoja wa kuupeleka mgogoro huo kwa jopo la maraisi wastaafu wa Afrika linaloongozwa na Joaquim Chissano Rais wa zamani wa Msumbiji ambalo linashughulikia kutatua hitilafu na migogoro mbalimbali barani  Afrika.
Pande hizo mbili zimeafikiana kwamba, iwapo hazitaridhishwa na maamuzi ya upatanishi huo, zitalazimika kuwasilisha hitilafu zao kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ. Malawi inadai kwamba mpaka wa nchi hizo mbili upo kwenye ufukwe wa Tanzania kwa maana kwamba nchi hiyo haina haki ya kutumia maji ya ziwa hilo ambalo linahesabiwa kuwa ni la tatu kwa ukubwa barani Afrika. Hii ni katika hali ambayo, Tanzania nayo inadai kuwa mpaka wa nchi hizo mbili uko katikati ya maji ya ziwa Nyasa. Mgogoro kati ya Tanzania na Malawi ulianza mwezi Julai mwaka huu baada ya Malawi kuanza kufanya utafiti wa mafuta katika eneo la Tanzania, hali ambayo ilisababisha serikali hizo mbili kuanza kulumbana. Inasemekana kuwa, chini ya maji ya ziwa hilo kuna utajiri mkubwa wa mafuta na gesi.

No comments:

Post a Comment