Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 20, 2012

BARUA YA MSAADA KWA WAISLAMU WOTE.............



JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU
(JUMIKI)
للجنة الدعوة الإسلامية
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
P. O. BOX: 1266 -Tel: +255-777-419473 / 434145-
FAX +255-024-2250022 E-Mail: jumiki@hotmail.com
MKUNAZINI ZANZIBAR

Ref. JMK/VOL/12/2012 05 Novemba, 2012
Bimillahir Rahmanir Rahiim

Ndugu Muislam,

YAH: OMBI LA MCHANGO WA MAAFA

Tafadhali husika na mada kama inavyosomeka hapo juu.

Kila sifa njema zinamstahikia Allah (S.W.T), rehma na amani zimuendee Mtume Muhammad (S.A.W), ahli zake, masahaba zake na waliowema katika Uislamu.

Kutokana na hali mbali mbali zilizojiri nchini mwetu hususan katika kuitetea Zanzibar huru yenye mamlaka yake kamili imepelekea baadhi ya watu kuathiriwa na hali hiyo ikiwemo kuuwawa kwa watu wasio na hatia, kuingiliwa majumbani mwao na kuibiwa mali zao na vyombo vya dola, pia wengine kuwekwa rumande wakiwemo Sheikh Msellem Ali, Amir Farid Hadi, Sheikh Khamis, Ustadh Hassan Bakar, Ustadh Ghalib na wengineo. Kutokana na hali hiyo jumuiya ya UAMSHO inakuomba uchangie kwa kadir ya ulivyojaaliwa na Allah (S.W.T) ili kuwasaidia waathirika hao, na ujira wako utaukuta siku yenye shida na hakutakua na msaada ila kwa kile ulichokitanguliza.

Tunamuomba Allah (S.W.T) akulipe badala na kilicho na kheri zaidi kwa unachokitoa.

Wabillahi Taufiq

KATIBU MKUU.
JUMUIYA YA UAMSHO.

No comments:

Post a Comment