Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, November 3, 2012

77 wauawa katika mapigano kusini mwa Sudan

77 wauawa katika mapigano kusini mwa Sudan
Wanajeshi 70 wa serikali ya Sudan na waasi saba wameuwawa kwenye mapigano makali yaliyojiri kati ya vikosi vya serikali ya Kharoum na waasi hao katika jimbo la Kordofan Kusini. Arnu Ngutulu  Msemaji wa harakati ya Sudan People's Liberation Movement – North ( SPLM-N) amesema kuwa, harakati hiyo kwa mara nyingine tena  imeshambulia kwa makombora mji wa Kadugli makao makuu ya jimbo hilo. Mashuhuda wameeleza kuwa,
idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo wamelazimika kuyakimbia makazi yao baada ya kushadidi mashambulizi. Ngutulu amesema kuwa, shambulio hilo la waasi limefanyika ikiwa  kulipa kisasi cha shambulio la anga lililofanywa na ndege za kivita za jeshi la serikali ya Khartoum kwenye vijiji vya Kordofan Kusini.  Serikali ya Sudan inaituhumu serikali ya Sudan Kusini kwa kuwapatia hifadhi pamoja na  silaha na zana za kivita waasi walioko kwenye mikoa ya Blue Nile, Kordofan Kusini na eneo la Darfur.

No comments:

Post a Comment