Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 18, 2012

Israel yaendeleza ukatili wake Ukanda wa Ghaza



Israel yaendeleza ukatili wake Ukanda wa GhazaUtawala haramu wa Israel umeendeleza ukatili wake kwa kuwaua shahidi Wapalestina wawili katika hujuma ya hivi karibuni  Ukanda wa Ghaza. Tayari Wapalestina karibu 50 wameuawa shahidi katika mashambulio ya  siku nne ya ndege za kivita za Israel dhidi ya watu wa Ghaza. Wanawake na watoto ndio whanaga wakubwa wa jina zinazoendelea za Israel dhidi ya Wapalestina huko Ghaza. Aidha katika hujuma ya hivi karibuni, ndege za kivita za Israel zimelenga jengo la mashirika ya habari mjini Ghaza ambapo waandishi habari sita wamejeruhiwa.
Wakati huo huo katika hatua ya kulipiza kisasi jinai za Israel, wanamapambano wa Palestina wamevurumisha makombora zaidi katika mji wa Tel Aviv.
Wakati huo huo viongozi wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu wamekutana mjini Cairo Misri na kusema wanaunga mkono Wapalestina katika kipindi hiki ambacho wanakabiliana na hujuma ya Israel. Hata hivyo viongozi hao wa nchi za Kiarabu wameshindwa kuchukua hatua za kivitendo za kukabiliana na ukatili wa Israel dhidi ya Wapalestina.

No comments:

Post a Comment