skip to main |
skip to sidebar
Israel yaendeleza ukatili wake Ukanda wa Ghaza
Utawala haramu wa Israel umeendeleza ukatili wake kwa kuwaua
shahidi Wapalestina wawili katika hujuma ya hivi karibuni Ukanda wa
Ghaza. Tayari Wapalestina karibu 50 wameuawa shahidi katika mashambulio
ya siku nne ya ndege za kivita za Israel dhidi ya watu wa Ghaza.
Wanawake na watoto ndio whanaga wakubwa wa jina zinazoendelea za Israel
dhidi ya Wapalestina huko Ghaza. Aidha katika hujuma ya hivi karibuni,
ndege za kivita za Israel zimelenga jengo la mashirika ya habari mjini
Ghaza ambapo waandishi habari sita wamejeruhiwa.
Wakati huo huo katika hatua ya kulipiza kisasi jinai za Israel,
wanamapambano wa Palestina wamevurumisha makombora zaidi katika mji wa
Tel Aviv.
Wakati huo huo viongozi wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu wamekutana
mjini Cairo Misri na kusema wanaunga mkono Wapalestina katika kipindi
hiki ambacho wanakabiliana na hujuma ya Israel. Hata hivyo viongozi hao
wa nchi za Kiarabu wameshindwa kuchukua hatua za kivitendo za
kukabiliana na ukatili wa Israel dhidi ya Wapalestina.
No comments:
Post a Comment