Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, November 3, 2012

Waasi wa Syria watumwa Saudia kufunzwa ugaidi


Waasi wa Syria watumwa Saudia kufunzwa ugaidi
Duru za habari zimeeleza kuwa, viongozi wa Saudi Arabia wamefanya kikao cha siri mjini Riyadh kwa shabaha ya kuyaongezea nguvu zaidi makundi ya waasi wanaobeba silaha dhidi ya serikali ya Syria. Toleo la leo la gazeti la al Quds al Arabi limeandika kuwa, viongozi wa Saudi Arabia na nchi nyingine za Kiarabu wamefanya kikao cha siri  na kufikia natija ya kutoa mafunzo zaidi ya kijeshi kwa waasi wa Syria kwa lengo la kutekeleza operesheni zaidi za  kigaidi nchini humo. Taarifa zinaeleza kuwa, kwenye kikao hicho imekubaliwa kwamba kundi la waasi wapatao elfu tatu lipelekwe katika eneo la Tabuk nchini Saudi Arabia kwa shabaha ya kupata mafunzo zaidi ya kijeshi na kutekeleza operesheni za kigaidi katika mikoa ya Idlib na Halab iliyoko kaskazini magharibi mwa Syria. Taarifa hizo zimeeleza kuwa, mafunzo hayo kwa magaidi, yatatolewa na maafisa wastaafu wa jeshi la Saudi Arabia yamelenga kuharibu miundombinu ya Syria.

No comments:

Post a Comment