Duru za habari zimeeleza kuwa, viongozi wa Saudi Arabia wamefanya
 kikao cha siri mjini Riyadh kwa shabaha ya kuyaongezea nguvu zaidi 
makundi ya waasi wanaobeba silaha dhidi ya serikali ya Syria. Toleo la 
leo la gazeti la al Quds al Arabi limeandika kuwa, viongozi wa Saudi 
Arabia na nchi nyingine za Kiarabu wamefanya kikao cha siri  na kufikia 
natija ya kutoa mafunzo zaidi ya kijeshi kwa waasi wa Syria kwa lengo la
 kutekeleza operesheni zaidi za  kigaidi nchini humo. Taarifa zinaeleza 
kuwa, kwenye kikao hicho imekubaliwa kwamba kundi la waasi wapatao elfu 
tatu lipelekwe katika eneo la Tabuk nchini Saudi Arabia kwa shabaha ya 
kupata mafunzo zaidi ya kijeshi na kutekeleza operesheni za kigaidi 
katika mikoa ya Idlib na Halab iliyoko kaskazini magharibi mwa Syria. 
Taarifa hizo zimeeleza kuwa, mafunzo hayo kwa magaidi, yatatolewa na 
maafisa wastaafu wa jeshi la Saudi Arabia yamelenga kuharibu miundombinu
 ya Syria.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment