Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, November 23, 2012

Wafuasi wa Rais Mursi waandamana hadi ikulu



Wafuasi wa Rais Mursi waandamana hadi ikulu
Mamia ya raia wa Misri wanaoumuunga mkono Rais Muhammad Mursi wa nchi hiyo leo wameandamana hadi katika ikulu ya rais wa nchi hiyo na kutangaza kuunga mkono uamuzi wake wa kumfukuza kazi mwendesha mashtaka mkuu na kuzuia  kuvunjwa baraza la kutunga katiba la nchi hiyo. Mamia ya Wamisri wanaomuunga mkono Rais Muhammad Mursi mapema leo wameandamana huku wakipiga nara za kumuunga mkono rais wao katika maamuzi aliyochukua  hapo jana ya kutangaza mabadiliko ya katiba ili kupanua uwezo wake. Rais wa Misri jana alitoa taarifa ya kisheria na kueleza kuwa hakuna chombo chochote cha kisheria kinachoweza kulivunja baraza la kutunga katiba la nchi hiyo. Mabadiliko hayo ya kisheria yanasisitiza kuhukumiwa upya Hosni Mubarak dikteta aliyeng'olewa madarakani huko Misri pamoja na viongozi wa zama za utawala wake wanaotuhumiwa kuwauwa wanamapinduzi na kufanya ufisadi katika uga wa kisiasa nchini humo.

No comments:

Post a Comment