Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 13, 2012

Israel inatumia silaha zilizopigwa marufuku, Palestina



Israel inatumia silaha zilizopigwa marufuku, PalestinaUtawala wa Kizayuni wa Israel unatumia silaha zilizopigwa marufuku zilizotengenezwa na Marekani kwa ajili ya kuua raia wa Palestina.
Kanali ya Televisheni ya Press imeripoti kuwa, utafiti uliofanyika unaonesha kwamba Israel inatumia silaha haramu zilizotengenezwa Marekani katika mashambulizi yake dhidi ya watu wa Gaza na Ukingo wa Magharibi.

Waziri wa Afya wa Palestina ametangaza pia kuwa askari wa Israel wanatumia silaha zilizopigwa marufuku zilizotengenezwa Marekani katika mashambulizi yake ya mara kwa mara katika Ukanda wa Gaza. Moja ya silaha zilizopigwa mrufuku kimataifa zinazotumiwa na Israel dhidi ya raia wa Palestina ni risasi zenye fosforasi nyeupe zilizotengenezwa Marekani ambazo Israel ilizitumia kwa wingi katika mashamabulizi yake ya mwaka 2009 katika Ukanda wa Gaza.
Mwanaharakati wa haki za binadamu wa Marekani Jo Carten anasema kuwa serikali ya Washington hutoa msaada wa zaidi ya dola bilioni tatu kwa Israel ikiwa ni pamoja na misaada ya silaha ambazo sehemu yake kubwa hutumiwa kushambulia wananchi wa Palestina.

No comments:

Post a Comment