Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, November 10, 2012

China kusaidia operesheni za kulinda amani Afrika

China kusaidia operesheni za kulinda amani Afrika
Serikali ya China imetoa msaada wa karibu euro milioni kumi kwa Umoja wa Afrika kwa shabaha ya kusaidia operesheni za vikosi vya kulinda amani barani humo. Makubaliano hayo yametiwa saini kati ya serikali ya China na Umoja wa Afrika yenye lengo la kudhamini gharama za maandalizi ya operesheni za kulinda amani barani humo. Erastus Mwencha Msaidizi wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amesema kuwa, msaada huo wa China utasaidia katika utekelezwaji wa operesheni ya umoja huo nchini Somalia, nchi ambayo kwa kiasi fulani imeshaanza kupata utulifu. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mwezi Novemba mwaka 2011, China ilikabidhi jengo jipya la Umoja wa Afrika nchini Ethiopia, makao makuu ya umoja huo.

No comments:

Post a Comment