Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, November 23, 2012

Mufti Mkuu wa Tanzania alaani jinai za Israel, Gaza



Mufti Mkuu wa Tanzania alaani jinai za Israel, GazaMufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Bin Shaaban Simba amelaaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza Palestina ambapo makumi ya  wanawake, watoto, wazee na vijana wasio na hatia wameuawa hivi karibuni kufuatia hujuma na amshambulio ya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza. Mufti Simba amesema, analaani mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya wananchi wa Palestina. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mufti Mkuu wa Tanzania amesema, anatoa wito kwa viongozi wa kitaifa na wale wa kimataifa, likiwemo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa kutafuta haraka suluhisho la kudumu la kadhia ya Palestina. Amesema, Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania BAKWATA siku zote limekuwa na itaendelea kuwa mstari wa mbele kuunga mkono harakati za Wapalestina za kupigania haki zao za kimsingi ikiwemo ya kuwa na nchi yao huru ya Palestina.

No comments:

Post a Comment