skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
Mufti Mkuu wa Tanzania alaani jinai za Israel, Gaza 
      
    
  
  
  
    
     
    
    
    
    
   
     Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Bin Shaaban Simba amelaaani 
jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza Palestina ambapo makumi
 ya  wanawake, watoto, wazee na vijana wasio na hatia wameuawa hivi 
karibuni kufuatia hujuma na amshambulio ya Israel dhidi ya Ukanda wa 
Gaza. Mufti Simba amesema, analaani mauaji yanayofanywa na Israel dhidi 
ya wananchi wa Palestina. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, 
Mufti Mkuu wa Tanzania amesema, anatoa wito kwa viongozi wa kitaifa na 
wale wa kimataifa, likiwemo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa 
kutafuta haraka suluhisho la kudumu la kadhia ya Palestina. Amesema, 
Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania BAKWATA siku zote limekuwa na 
itaendelea kuwa mstari wa mbele kuunga mkono harakati za Wapalestina za 
kupigania haki zao za kimsingi ikiwemo ya kuwa na nchi yao huru ya 
Palestina.
Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Bin Shaaban Simba amelaaani 
jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza Palestina ambapo makumi
 ya  wanawake, watoto, wazee na vijana wasio na hatia wameuawa hivi 
karibuni kufuatia hujuma na amshambulio ya Israel dhidi ya Ukanda wa 
Gaza. Mufti Simba amesema, analaani mauaji yanayofanywa na Israel dhidi 
ya wananchi wa Palestina. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, 
Mufti Mkuu wa Tanzania amesema, anatoa wito kwa viongozi wa kitaifa na 
wale wa kimataifa, likiwemo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa 
kutafuta haraka suluhisho la kudumu la kadhia ya Palestina. Amesema, 
Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania BAKWATA siku zote limekuwa na 
itaendelea kuwa mstari wa mbele kuunga mkono harakati za Wapalestina za 
kupigania haki zao za kimsingi ikiwemo ya kuwa na nchi yao huru ya 
Palestina.
    
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment