Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, November 9, 2012

Viongozi wa Kiislamu Tanzania wabakia rumande

Viongozi wa Kiislamu Tanzania wabakia rumandeMahakama za Tanzania zimeendelea kuwashikilia jela viongozi kadhaa wa Kiislamu nchini humo. Huko visiwani Zanzibar, Amiri wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar Sheikh Farid Hadi na masheikh wengine kadhaa akiwemo Sheikh Mselem Ali Mselem na Sheikh Azan Khalid Hamdan wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu JUMIKI wameendelea kubakia rumande baada ya kuwekewa masharti mazito ya dhamana. Huku hayo yakiripotiwa, mawakili wa viongozi hao wa taasisi za Kiislamu Zanzibar wamelalamika vikali kuwa wateja wao wanavunjiwa haki ikiwa ni pamoja na kunyolewa ndevu bila ya ridhaa zao wakiwa rumande.
Hati ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar ndiyo iliyotumika kuendelea kuwaweka rumande masheikh hao. Vile vile jana Alkhamisi mkurugenzi wa mashtaka Tanzania Bara (DPP) aliendelea kumuweka rumande Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Shekhe Ponda Issa Ponda. Miongoni mwa mashtaka yanayowakabili viongozi hao wa taasisi za Kiislamu Tanzania ni uchochezi na kusababisha fujo na uvunjifu wa amani. Taarifa nyingine zinasema kuwa Waislamu 49 wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania wameachiliwa huru kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment