skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
Viongozi wa Kiislamu Tanzania wabakia rumande 
      
    
  
  
    
     
    
    
    
    
   
    
 Mahakama za Tanzania zimeendelea 
kuwashikilia jela viongozi kadhaa wa Kiislamu nchini humo. Huko visiwani
 Zanzibar, Amiri wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar Sheikh Farid Hadi na 
masheikh wengine kadhaa akiwemo Sheikh Mselem Ali Mselem na Sheikh Azan 
Khalid Hamdan wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu JUMIKI 
wameendelea kubakia rumande baada ya kuwekewa masharti mazito ya 
dhamana. Huku hayo yakiripotiwa, mawakili wa viongozi hao wa taasisi za 
Kiislamu Zanzibar wamelalamika vikali kuwa wateja wao wanavunjiwa haki 
ikiwa ni pamoja na kunyolewa ndevu bila ya ridhaa zao wakiwa rumande.
Mahakama za Tanzania zimeendelea 
kuwashikilia jela viongozi kadhaa wa Kiislamu nchini humo. Huko visiwani
 Zanzibar, Amiri wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar Sheikh Farid Hadi na 
masheikh wengine kadhaa akiwemo Sheikh Mselem Ali Mselem na Sheikh Azan 
Khalid Hamdan wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu JUMIKI 
wameendelea kubakia rumande baada ya kuwekewa masharti mazito ya 
dhamana. Huku hayo yakiripotiwa, mawakili wa viongozi hao wa taasisi za 
Kiislamu Zanzibar wamelalamika vikali kuwa wateja wao wanavunjiwa haki 
ikiwa ni pamoja na kunyolewa ndevu bila ya ridhaa zao wakiwa rumande.  
Hati ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar ndiyo iliyotumika kuendelea 
kuwaweka rumande masheikh hao. Vile vile jana Alkhamisi mkurugenzi wa 
mashtaka Tanzania Bara (DPP) aliendelea kumuweka rumande Katibu wa 
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Shekhe Ponda Issa Ponda. 
Miongoni mwa mashtaka yanayowakabili viongozi hao wa taasisi za Kiislamu
 Tanzania ni uchochezi na kusababisha fujo na uvunjifu wa amani. Taarifa
 nyingine zinasema kuwa Waislamu 49 wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu 
Tanzania wameachiliwa huru kwa dhamana.
    
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment