Rais Macky Sally wa Senegal amesema kuwa hatafanya mazungumzo ya 
aina yoyote na waasi wa eneo la Casamance yenye lengo la kujitenga na 
serikali kuu ya nchi hiyo. Akizungumza kwenye kongamano la wakurugenzi 
wa vyombo vya habari vya Afrika mjini Dakkar, Rais Sally ameongeza kuwa,
 kujitenga eneo la Casamance kamwe jambo halikubaliki na kusisitiza 
kwamba Casamance ni sehemu ya ardhi ya Senegal. Ameongeza kuwa, njia 
pekee ya kuutatua mgogoro wa eneo hilo lililopo kusini mwa nchi hiyo ni 
kuendelezwa mazungumzo kati ya serikali na waasi wa The Movement of 
Democratic Forces of Casamance MFDC. Rais wa Senegal amebainisha kuwa, 
kufanyika mazungumzo ya wazi kwa shabaha ya kupatikana amani na 
uthabiti, kutapelekea kupatikana ustawi na maendeleo ya kiuchumi nchini 
humo. Waasi wa Casamance walianza uasi tokea miaka ya 1980  kwa  lengo 
la kujitenga eneo la kusini mwa nchi hiyo.  Inafaa kukumbusha kuwa, 
Abdullaye Wade Rais wa zamani wa Senegal alifikia kwenye makubaliano ya 
amani na waasi hao wa MFDC.
   
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







 

 
 
 
 
 





 
 







No comments:
Post a Comment