Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 11, 2012

Rais Sally apinga kujitenga Casamance



Rais Sally apinga kujitenga Casamance
Rais Macky Sally wa Senegal amesema kuwa hatafanya mazungumzo ya aina yoyote na waasi wa eneo la Casamance yenye lengo la kujitenga na serikali kuu ya nchi hiyo. Akizungumza kwenye kongamano la wakurugenzi wa vyombo vya habari vya Afrika mjini Dakkar, Rais Sally ameongeza kuwa, kujitenga eneo la Casamance kamwe jambo halikubaliki na kusisitiza kwamba Casamance ni sehemu ya ardhi ya Senegal. Ameongeza kuwa, njia pekee ya kuutatua mgogoro wa eneo hilo lililopo kusini mwa nchi hiyo ni kuendelezwa mazungumzo kati ya serikali na waasi wa The Movement of Democratic Forces of Casamance MFDC. Rais wa Senegal amebainisha kuwa, kufanyika mazungumzo ya wazi kwa shabaha ya kupatikana amani na uthabiti, kutapelekea kupatikana ustawi na maendeleo ya kiuchumi nchini humo. Waasi wa Casamance walianza uasi tokea miaka ya 1980  kwa  lengo la kujitenga eneo la kusini mwa nchi hiyo.  Inafaa kukumbusha kuwa, Abdullaye Wade Rais wa zamani wa Senegal alifikia kwenye makubaliano ya amani na waasi hao wa MFDC.

No comments:

Post a Comment