Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, November 8, 2012

Wanafunzi USA wapinga ushindi wa Obama


Wanafunzi USA wapinga ushindi wa Obama
Duru za habari kutoka Marekani zimearifu kuwa, mamia ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Mississippi katika jimbo la Mississipi, wamefanya maandamano makubwa kupinga ushindi wa Rais Barack Obama. Wanafunzi hao wanaokadiriwa kufikia 400 walimiminika mabarabarani kupinga hatua ya kuchaguliwa mara ya pili rais Obama. Chuo kikuu hicho kimetoa ripoti kuwa, mikusanyiko ya wanafunzi ilianza tangu siku ya Jumanne usiku na kuongezeka zaidi jana na leo. Wanafunzi hao waliokuwa wamejawa na hasira walibeba mabango mbalimbali huku wengine wakitoa nara za kulaani ushindi huo wa Obama. Kufuatia purukushani hizo, polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wanafunzi hao.

No comments:

Post a Comment