skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
 UNICEF yalaani utekaji nyara nchini Kongo
    
     
    
    
    
    
   
Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umelaani vikali hatua 
ya kukamatwa mateka wafanyakazi wawili wa sekta ya afya katika eneo 
linalokumbwa na machafuko la Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya 
Kidemokrasia ya Kongo. Taarifa ya UNICEF imeeleza kuwa, mhandisi mmoja 
anayeshughulikia na masuala ya ustawi wa ujenzi na mwengine mtoa misaada
 ya kibinadamu katika jimbo hilo, wamekamatwa mateka na watu wanaobeba 
silaha karibu wa mpaka wa nchi hiyo na Uganda. Taarifa hiyo imeongeza 
kuwa, wafanyakazi hao wamekamatwa mateka wakati wakitoa chanjo za polio 
kwa watoto katika eneo hilo. UNICEF imeeleza kuwa, kutolewa  huduma 
likiwemo suala la kupatiwa chanjo watoto wadogo, ni miongoni mwa haki za
 watoto wote ulimwenguni. Jumla ya watu milioni mbili na nusu 
wanakabiliwa na hali mbaya ya kiafya kwenye kambi za wakimbizi zilizopo 
kwenye eneo la mashariki mwa Kongo
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment