Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 11, 2012

UNICEF yalaani utekaji nyara nchini Kongo


UNICEF yalaani utekaji nyara nchini Kongo
Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umelaani vikali hatua ya kukamatwa mateka wafanyakazi wawili wa sekta ya afya katika eneo linalokumbwa na machafuko la Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Taarifa ya UNICEF imeeleza kuwa, mhandisi mmoja anayeshughulikia na masuala ya ustawi wa ujenzi na mwengine mtoa misaada ya kibinadamu katika jimbo hilo, wamekamatwa mateka na watu wanaobeba silaha karibu wa mpaka wa nchi hiyo na Uganda. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, wafanyakazi hao wamekamatwa mateka wakati wakitoa chanjo za polio kwa watoto katika eneo hilo. UNICEF imeeleza kuwa, kutolewa  huduma likiwemo suala la kupatiwa chanjo watoto wadogo, ni miongoni mwa haki za watoto wote ulimwenguni. Jumla ya watu milioni mbili na nusu wanakabiliwa na hali mbaya ya kiafya kwenye kambi za wakimbizi zilizopo kwenye eneo la mashariki mwa Kongo

No comments:

Post a Comment