Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 11, 2012

Syria bila ya Assad itakuwa kitovu cha magaidi



Syria bila ya  Assad itakuwa kitovu cha magaidiMchambuzi mmoja wa masuala ya kisiasa ameonya kuwa iwapo wapiganaji wa Kisalafi wanaopigana vita dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wataidhibiti Syria, basi nchi hiyo ya Kiarabu itageuka na kitovu cha mazalio ya magaidi katika eneo la Mashariki ya Kati. Dakta Ismail Salami msomi wa Kiirani na mchambuzi wa masuala ya kisiasa katika eneo hili amesema ni wazi kuwa wanamgambo wa Kisalafi tayari wapo huko Syria na wanaendesha mapigano dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo. Akiashiria wito uliotolewa mwezi Februari mwaka jana  na Ayman al Zawahiri kiongozi wa mtandao wa al Qaida kwa wafuasi wake akiwataka waendeshe vita dhidi ya Rais wa Syria, Dakta Ismail Salami amesema kuwa lengo kuu la njama hizo ni kuigeuza Syria kuwa maficho salama kwa Masalafi.

No comments:

Post a Comment