
Jenerali Nyakairima ameongeza kuwa, Rais Joseph Kabila wa Kongo siku ya Jumamosi tarehe 24 Novemba alikutana na kufanya mazungumzo na mwakilishi wa waasi wa M23 mjini Kampala, Uganda na kuwapa sharti la kuondoka kwanza na kurejea nyuma hadi kwenye mji wa Sake ulioko umbali wa kilomita 20 kutoka Goma kabla ya kufanyika mazungumzo ya amani.
Hivi karibuni, Wakuu wa nchi wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu ya Afrika ICGLR walikutana mjini Kampala, na kuchukua uamuzi wa kuwapa muda wa masaa 48 waasi hao kuondoka mji wa Goma, makao makuu ya jimbo la Kivu Kaskazini.
No comments:
Post a Comment