Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 14, 2012

107 wafariki kwa homa ya manjano Darfur, Sudan



107 wafariki kwa homa ya manjano Darfur, Sudan
Mripuko wa homa ya manjano huko katika jimbo la Darfur nchini Sudan umeua watu 107 katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hayo yameripotiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na kutahadharisha kwamba ugonjwa huo huenda ukaenea kote nchini Sudan. WHO imesema kuwa homa hiyo ya manjano inazidi kuua watu wengi na kwamba Sudan hivi sasa inafanya juhudi za kupata chanjo ya dharura ya maradhi hayo. Maafisa wa WHO waliripoti kuwa jumla ya watu 67 wamefariki dunia kwa maradhi hayo ya homa ya manjano. Hakuna dawa maalumu kwa ugonjwa wa homa ya manjano inayoenezwa na mbu, bali daktari humhudumia mgonjwa kulingana na dalili kuu anazokuwa nazo kama vile  kuwa na upungufu wa maji mwilini, homa, kuvuja damu na kutapika. Dakta Ansu Banerjee wa Ofisi ya WHO huko Sudan amesema kuwa jumla ya dozi milioni 2.4 za chanjo ya homa ya manjano zinatazamiwa kuwasili Khartoum mji mkuu wa Sudan wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment