Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 28, 2012

'Israel inakiuka haki za binaadamu za Wapalestina'


  •  
'Israel inakiuka haki za binaadamu za Wapalestina'
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amelaani hatua ya Israel ya kukiuka haki za binadamu katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina. Nabil al Arabi amesema hayo leo alipokutana na Richard A. Falk Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina kwenye makao makuu ya jumuiya hiyo mjini Cairo. Al Arabi amelaani hatua za askari wa Israel za kukiuka haki za binadamu katika ardhi za Palestina ukiwemo Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu pia ameunga mkono aumuzi wa Wapalestina wa kutaka kuwa na uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, pendekezo ambalo linatarajiwa kupigiwa kura hapo kesho katika kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.  Wakati huo huo Muhammad Swabih, Naibu Katibu Mkuu wa Arab League anayeshughulikia masuala ya Palestina amesema kwamba, safari ya Richard Falk mjini Cairo ni muhimu na kusisitizia udharura wa kuungwa mkono mapendekezo na maazimio ya kimataifa kuhusiana na taifa la Palestina.

No comments:

Post a Comment